
Akizungumza na wahitimu wa ngazi ya
uwalimu wa maandalizi katika mahfali ya pili ya mradi wa ‘' watoto kwanza ''
huko katika ukumbi wa sameil academy gombani chake chake Pemba Naibu Warizi wa
elimu na mafunzo ya Amali Zanzibar Mh. Mmanga Mjengo Mjawiri amesema Serekali
imekabiliwa na changamoto ya ukosefu wa walimu wa maandalizi hivyo kupitia
wahitimu hao wataweza kutoa ajira ili kuleta mabadiliko makubwa katika maeneo
yao.
Amesema upungufu wa walimu wa maandalizi
upo na sasa kuna pengo kubwa amabalo linafikia zaidi ya 536 kupitia wahitimu
hao wataweza kutoa ajira ili kuziba pengo ambalo linaonekana kudhofisha
wanafunzi wa maandalizi hapa Zanzibar.
Amesema ili mwalimu awezekuleta
mabadiliko nivyema abadilike kwakutoa elimu inayo endana na wakati nakuweza
kutanua wingo mpana kwa wananfunzi.
Aidha amewaomba wahitimu hao kuyatumikia
vizuri mafunzo walioyapata ili iwe matunda bora kwa wanafunzi wa maandalizi
wamaokwenda kuwatumikia.
Kwaupande wake mkurugenzi wa Madrasa
Early Childhood Programme Zanzibar Nd.Khamis Abulla Said amesema licha ya kuwepo changamoto mbali mbali
zinazo wakabili katika kutoa taaluma kwa walimu lakini bado wanaendelea
kupambana nanzo.
Amefahamisha kuwa kwa kushirikiana na
shirika la UNICEF agakan fodation na Dubai care wameweza kufadhili mafunzo mbali
mbali ambayo yamewasaidia kutoa elimu kwa walimu wa maandalizi wapatao 970.

Comments