Akizungumza na Zanzibar24 kufuatia wazazi kulalamika kutozwa michango katika skuli hiyo amesema kuwa michango inayotozwa kwa wanafunzi ni kutokana na kuwepo kwa upungufu wa vyoo katika skuli hiyo.
Amesema kuwa kuna baadhi ya wananchi hawana utamaduni wa kutoa michango midogo midogo katika skuli hali ambayo inazorotesha maendeleo ya skuli hiyo.
Aidha Mkuu huyo amefahamisha kuwa Wilya hiyo imeandaa mpango wa kutoa elimu kwa wazazi na walezi juu ya kutoa michango ambayo itasaidia katika skuli mbalimbali ili kukabiliana na matatizo yanayojitokeza.
chanzo:Zanzibar24
Comments