Watu 6 washikiliwa na polisi kwatuhuma zakupatikana na magunia 26 ya karafuu.

Image result for newsWatu sita  wanashikiliwa na jeshi la polisi mkoa kusini pemba kwa tuhuma zakupatikana na magunia 26 ya karafuu kavu katika mazingira tofauti yanayo tilia shaka kuwa walikuwa wikizipeleka mahala pasipo julikana.

.kwa mujibu wa tarifa ilio tolewa na kamanda wa polisi mkoa kusini pemba kamishina msaidizi mwandamizi Mohamed Shekhani Mohamed amesema gunia 16 wamezikamata zikiwa ndani ya gari ya Noha majira ya saa 2 usiku ikiwa imegesha karibu na kivuko cha ukaguzi wa karafuu ngwachani na gunia 10 wamezikamata zikisadikiwa kuwa wamiliki wamenunua kwa njia isio halalali.


Amesema karafuu hizo tayari zimepelekwa katika shirika la zstc zimepimwa na kufikia kilo 1410.5 zenyethamani ya ziadin ya sh milioni 18 waolizo shikwa nazo watuhumiwa hao.

Mapema mkuu wamkoa kusini pemba bimwanajuma majidi abdala akiwa katika shirika la zstc kushhudia makabidhiano ya karafuu hizo amesema inaonekana kuna wakulima bado hawaja taka kufata sheria na utaratibu hivyo kuanzia sasa watafanya msako wa nyumba kwanyumba kuhakikisha karafuu zote zinapelekwa katika shirika la zstc.

Kwa upandewake mkuu wa wilya chake amawataka wakulima kuacha kuza karafuu kwa watu  wakawaida kwani licha ya kuwa nikinyume na sheria lakini pia pishi wanazo uzia zinawapunuja.

.Baadhi ya watuhumiwa hao  wakishuhudia karafuu zao kukabidhiwa shirika la zstc wakiwa kwenye ulinzi mkali wa wavyombo vy ulinzi wamesema wao hukusanya karafuu hizo nakisha  kuzi peleka kuuza shirika la zstc wakitegemea kupata faida kidogo.

 chanzo:zanzibar24.

Comments