Ucheleweshaji wa upepelezi na ukosefu wa umakini katika ushahidi chanzo cha kushindwa kwa kesi nyingi

Hakimu Moh’d ametoa kauli hiyo huko katika makao makuu ya
polisi Tunguu wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya wiki mbili kwa
maafisa na askari wa jeshi la polisi mkoani humo yenye lengo la
kuwajengea uwezo ili waweze kuleta ufanisi katika utekelezaji wa
majukumu yao ya kila siku.
Amesema kumekuwa na mrundikano wa kesi nyingi katika mahakama za
wilaya na mkoa ambazo zinajumuisha makosa mbali mbali yakiwemo ya
ubakaji, kutorosha, madawa ya kulevya, ulawiti na ajali za barabarani
jambo ambalo linapelekea kurudhisha nyuma juhudi za mahakama katika
kuwapatia wananchi haki zao.
Aidha amewataka askari wa jeshi hilo kuzitambua na kuzifanyia kazi
sheria zinazohusiana na makosa mbali mbali yakiwemo makosa ya jinai ili
kuona kwamba wanaleta mabadiliko makubwa ndani ya jeshi hilo.
Nae akizungumza kwa niaba ya kaimu kamishna wa polisi zanzibar
kamishna msaidizi mwandamizi wa polisi ndugu Saleh Mohd Saleh amesema
umefika wakati wa askari wa jeshi la polisi kuondokana na kufanya kazi
zao kwa kubahatisha na badala yake kuzingatia maadili na ueledi wa kazi
zao ili kuona kwamba wanaondosha malalamiko kwa wanachi.
Kwa upande wa kamanda wa polisi mkoani humo ndugu Makarani Khamis
Ahmeid amesema jeshi la polisi limeamua kutoa mafunzo kwa askari wake
baada ya kuona lina mapungufu na changamoto mbali mbali za kiutendaji.
Chanzo:zanzibar24.
Comments