
Akitoa taarifa kuhusu maandalizi ya Uchaguzi huo amevitaka vyama vya
siasa kuhakikisha kuwa vinawaelemisha wafuasi wao kwani iwapo wafuasi wa
vyama vya siasa watavunja maadili, chama husika pamoja na mgombea wake
kitachukuliwa hatua za kinidhamu.
Miongoni mwa vitendo vinavyokiuka maadili ya uchaguzi ni pamoja na
wagombea au wafuasi wa vyama hivyo kuchana mabango ya wagombea wengine,
kutoa lugha chafu wakati wa mikutano ya kampeni pamoja na kupitisha muda
wa kufanya mikutano ya kampeni.
Amezitaka kamati za maadili za kata na jimbo kuchukua hatua kali
ndani ya masaa 48 pindi vitendo hivyo vikijitokeza na adhabu itakuwa
ni kuomba radhi wananchi hadharani, kutotumia vyombo vya habari kwa muda
fulani, onyo la maandishi kusimamishwa kufanya kampeni, mgombea
kutangaza mbele ya vyombo vya habari kuwa yeye ni bingwa wa kuvunja
maadili ya uchaguzi au kutozwa faini Sh 100,000.
Kailima pia amesema chama kitakachotaka kufanya mabadiliko ya ratiba
ya mikutano ya kampeni, lazima kimfahamishe msimamizi wa uchaguzi wa
kata na ombi hilo litajadiliwa na vyama vyote vinavyoshiriki kwenye
uchaguzi.
Vitambulisho mbadala vitakavyotumika kupigia kura kwa wale ambao
wamepoteza kadi ya mpiga kura ni vitambulisho vya taifa, leseni ya
udereva na hati ya kusafirisha hata kama vimeisha muda wake, mhusika
anaruhusiwa kupiga kura.
Wakati huo huo, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imesema kuwa katika
uchaguzi mdogo wa madiwani utakaofanyika Novemba 26, 2017 katika kata 43
utagharimu kiasi cha Sh bilioni 2.5.
chanzo: zanzibar24.
Comments