MUWASA – Usambazaji wa maji utakamilika Dec, 30, 2017.

Mamlaka ya maji safi na mazingira mjini Musoma (MUWASA) imewahakikishia wananchi wa manispaa ya Musoma kuwa mradi mkubwa wa maji kupitia mfumo mpya wa usambazaji wa huduma hiyo unataraji kukamilika kwa asilimia mia moja ifikiapo Dec. 30 mwaka huu.

Hayo yamesemwa na meneja ufundi wa mamlaka ya maji safi MUWASA mhandis BURTON MAJIGILI amesema hayo alipokua akitoa ufafanuzi wa ukamilishwaji wa mradi mkubwa wa maji wa Bukanga katika kikao cha madiwani hivi karibuni.


Mhandisi MAJIGILI amesema kutokamilika kwa mardi huo kwa muda uliopangwa kumetokana na kazi kubwa ya kubadilisha mfumo wa Zamani wa kusambaza maji na kuweka mfumo mpya wa mabomba ya usambazaji maji ambao unataraji kukamilika mwezi Dec. 30 mwaka huu na hivyo kutoa matumaini mapya yanayolenga kuondoa tatizo la maji linaloikabili manispaa ya musoma kwa muda mrefu sasa.

Hata hivyo kauli za kukamilishwa kwa mradi huo mkubwa wa maji zimepokelewaje na madiwani hao ambao kiu yao ni kuona wananchi wao wanaandokana na adha ya ukosefu wa maji safi na salama.

chanzo:zanzibar24.

Comments