Mkutano wa kumi na nne wa Chama Cha Waandishi wa Habari Zanzibar kufanyika disembe 16.

Image result for Waandishi wa HabariMkutano wa kumi na nne wa Chama Cha Waandishi wa Habari Zanzibar ZPC unatarajiwa kufanyika disembe 16 mwaka huu ambapo mkutano utazungumzia namna upatikanaji wa habari sahihi katika jamii ambazo zinatasidia ukuwaji wa uchumi.

Akizungumza na waandishi wa habari kuhusiana na Mkutano huo Mwenyekiti wa Chama cha waandishi wa habari ZPC Abdallah Abdlrahman mfaume amesema kutokana na vyombo vya habari kuwa na uwezo mkubwa wa kuimarisha ukuwaji wa Uchumi Nchini ni vyema kuendelea kushirikishwa katika utoaji wa taarifa muhimu.


Amesema kutokana na Serikali ya Zanzibar kuwa katika harakati za kufikia uchumi wa kati Mkutano huo pia utawapa fursa waandishi wa habari kujifunza dhana ya uchumi wa viwanda na uchumi wa kati katika kuandika habari zitakaimarisha maendeleo Nchini.

Aidha amesema mkutano huo pia utaifanyia marekebisho katiba ya mwaka 2003 ili iweze kuendana na matakwa na mahitaji wa wananachama katika kuendeleza ufanisi wa kufanya kazi katika jamii.

Hata hivyo ametowa wito kwa waandishi wa habari kuendeleza mashirikiano katika utendaji wa kazi zao pamoja na kujiunga na chama hicho ili kunufaika na fursa zilizopo ikiwemo kushiriki mafunzo ya kuengeza ufanisi katika utendaji wa kazi zao.

Kwa upande wake Kaimu katibu mkuu wa Chama hicho Mwinyi Mvua Abdi Nzukwi amesema licha ya mafanikio  yaliopatikana chama hicho lakini kumekuwa na tatizo la ushiriki mdogo wa Waandishi wa habari katika kuendeleza chama hicho.

Amesema ili kufikia malengo yaliyokusudiwa ni vyema kwa waandishi wa habari kuwa mstari wa mbele katika kukiendeleza chama hicho pamoja na kuendelea kuandika habari zenye ukweli katika kuendeleza amani iliopo.

Mkutano huo unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa na kimataifa ambapo waziri wa fedha na Mipango anatarajiwa kuwa Mgeni Rasmin katika mkutano huo wenye ujumbe usemao Vyombo vya Habari ni Chachu ya kufikia Uchumi wa Viwanda Vishirikishwee.

chanzo:zanzibar24.

Comments