
Tukio hilo lilitokea juzi asubuhi majira ya saa 3:30 Mjimkongwe wilaya ya mji.
Akithibitisha kutikea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mjini
Maghari, Hassan Nassir Ali, alisema kijana huyo alitiwa mikononi akiwa
katika harakati za kumfanyia mtihani, Rukia Bukuku Laurence ambae ni
mjamzito.
Alisema baada ya uchunguzi kukamilika mtuhumiwa huyo atafikishwa katika vyombo vya sheria kujibu tuhuma zinazomkabili.
Ofisa Elimu mkoa huo, Khatib Tabia Muhsin, akizungumzia kadhia hiyo
alisema suala la udanganyifu wa mtihani lina athari kubwa kwa skuli na
mwanafunzi hivyo akawataka kujiepusha.
Kuhusu madai ya kuwepo wanafunzi sita katika skuli ya Mpendae
kuzuiliwa kufanya mtihani wa kemia, alisema madai hayo si ya kweli na
wanafunzi wanaendelea kufanya mitihani yao kama kawaida.
Kuhusu wanafunzi wanoshindwa kufanya mitihani kwa sababu ya kuumwa,
alisema taratibu zimewekiwa ikiwemo mzazi kwenda kwa daktari aliyemtibu
mwanafunzi huyo na kumuandikia barua kuhusu ugonjwa wake ili hatua
zichukuliwe.
Chanzo: ZanzibarLeo na zanzibar24.
Comments