Chinjio lafungwa kutokana na kutoridhisha mazingira yake.

HABARIMkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya kaskazini B Fatma Mohammed Juma amesema kufungiwa  kutoa huduma kwa chinjio  la donge Muwanda kunatokana  na  mfumo uliopo wa maji machafu kutoridhisha.

Akizungumza na Zanzibar24  amesema Mfumo  huo  haukuwa salama  kiafya  jambo ambalo  lingepelekea   kutokea kwa  maradhi katika chinjio hilo.


Aidha amefahamisha kuwa hivi sasa wanampango  wa kulifanyia matengenezo  yatakayolifanya  chinjio hilo kuwa  na kiwango cha kuridhisha  ambalo halitoathiri mazingira ya eneo hilo na watumiaji.

Hata hivyo  amewataka wafanyabiashara  wa   nyama  kufuata  sheria  na kutumia  machinjio   yaliyothibitishwa  kitaalamu ili  waweze  kuchinja wanyama  wao katika sehemu  salama na safi kwa matumizi ya mwanadamu.

chanzo:Zanzibar24

Comments