Waziri Makamba amjibu Ally Saleh kuhusu ziara yake ya Zanzibar.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais  Muungano na Mazingira Mhe January Makamba amemjibu Mbunge wa Mji mkongwe ambaye pia ni Waziri kivuli anaeshughulikia masuala ya Muungano Ally Saleh  madai yake ya kutokujulishwa ujio wa Waziri huyo visiwani hapa.

Awali kupitia ukurasa wake wa Twitter Mbunge Ally Saleh alimlaumu Waziri Makamba kuwa amekuja Zanzibar kushughulikia kero za Muungano lakini yeye kama Waziri kivuli hakujua chochote kwa kutofahamishwa kuhusu ujio huo.


Nae Waziri Makamba kupitia mtandao huohuo wa Twitter alimjibu Waziri Makamba kuwa itakua vigumu kwa kila Waziri anapofanya kazi kumjulisha Waziri kivuli lakini alitumia nafasi hiyo kukiri kughafilika kwake kumjulisha Mbunge huyo kama rafiki na mdau wa mambo ya muungano.

Waziri Makamba yupo katika ziara ya kikazi visiwani hapa kwa muda wa siku saba akiwa amejikita zaidi kushughulikia masuala ya uchumi ikiwa ni pamoja na masuala ya Bandari, Forodha, Kodi na kubaini changamoto zilizopo, utekelezaji wa maazimio yaliyokubaliwa katika vikao vya majadiliano na kuangalia maeneo mapya yanayohitaji kuingizwa katika mfumo wa utatuzi.

chanzo: zanzibar24.

Comments