Wazanzibar watolewa hofu kuhusu upungufu wa Petroli nchini.

KAIMU Mkurugenzi Huduma kwa Wateja Mussa Ramadhan Haji amesema kuwa tatizo lilotokea la upungufu wa mafuta  ni la muda mfupi kutokana na vituo vya GAPCO  na ZP kutokuwa na mafuta ya petrol.

Hayo ameyasema  huko katika ofisi zao zilizopo Maisara wakati akitoa ripoti kwa waandishi wa habari kuhusu uvumi  uliojitokeza nchini wa upungufu wa huduma hiyo.


Alisema  kuwa kwa sasa Zanzibar mafuta yapo ya kutosha lita Milion 1. 7 za Petrol zipo na kwa siku zaidi ya lita 165,000  ya petrol ni mahitaji ya matumizi ya mafuta,na idadi hiyo inaweza kutosheleza zaidi  kwa matumizi Zanzibar  kwa  siku kumi na moja.

Aidha aliwatoa hofu wananchi kwa kusema kuwa meli ya mafuta ipo njiani baada ya siku 4 itaingia nchini na kushusha mafuta ya kutosha.

“ Serikali inasimamia vyema kuhakikisha mapungufu haya hayaendelei na kuwathibitishia wananchi  mafuta yapo ya kutosha na bei zile zile zilizokuwepo  kama kawaida”Alisema kaimu huyo.

Aidha amewataka wananchi waache kununua mafuta kwa njia ya magendo ili kuuza kwa bei iliyokuwa si halali ambayo imethibitishwa na Serikali.

chanzo: zanzibar24.

Comments