Vifaa vitakavyotumika kuimarisha bandari ya Dar es Salam vyawasili nchini.

Meneja wa bandari ya Dar es Salaam Bw. Fred Liundi amesema  vifaa vitakavyotumika kwa ajili ya mradi wa kupanua bandari ya Dar es Salam ili kuipa uwezo bandari hiyo kuhudumia  meli kubwa kutoka urefu wasasa wa meta 243 hadi kufikia  urefu wa meta 320,teri vimesha wasili nchini.

Upanuzi wa bandari hiyo unafanywa na kampuni ya China Harbour  Enginering  CO kutoka nchini China, chini ya usimamizi wa Bi.Anastazia  Saled, ambapo mbali na kuongezwa kina cha Bandari pia watajenga gati mpya  kwa  ajili ya kushusha magari.


Aidha Meneja huyo amewatoa wasiwasi watumiaji wa bandari hiyo kuwa ujenzi huo hautaadhiri utoaji wa huduma zozote zile bandarini hapo.

 chanzo:zanzibar24.

Comments