
Akijibu Swali katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi Chukwani nje
kidogo ya Mji wa Zanzibar Waziri wa fedha na Mipango Dk. Khalid Salum
amesema ni kweli kwa muda Mrefu jengo hilo halijaendelezwa lakini hatua
za awali za uendelezaji wa Jengo hilo umenza.
Amesema maafisa kutoka UNESCO tayari wapo nchini kwa ajili ya ukaguzi
wa miradi iliopo katika Maeneo mbali mbali ya Urithi wa Mji mkongwe
ikiwemo Jengo la Hoteli ya Bwawani , Bet al jaib na koridoo za darajani
ili kuzipatia vibali vya kuendeleza majengo hayo.
Akizungumzia sababu za kuchelewa kwa jengo hilo Dk. Khalid amesema ni
pamoja na kutokamilika kwa wakati kwa tathmini za kimazingira
kumechangia kuchelewa kwa ujenzi huo.
Amesema Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea na jitihada za
kumharakisha muekezaji ili ukarabati huo uweze kukamilika kwa wakati
katika kuimarisha maendeleo Nchini.
Hoteli hiyo imekodishwa kwa kampuni ya Quality Group ya Dar es Salaam
november 17 -2015 .
chanzo:Zanzibar24.
Comments