Spika wa Bunge atolea maelezo barua ya Mbunge wa Singida Kaskazini Nyalandu.

spikaSijapokea barua ya Mbunge wa Singida Kaskazini kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM), Lazaro Nyalandu kuhusu uamuzi wake wa kujiuzulu ubunge.

Hayo yamesemwa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai wakati akifanya mahojiano na kituo cha Azam.


Spika Ndugai alisema ingekuwa vizuri kama kiongozi Lazaro Nyalandu angewasilisha kwanza barua hiyo katika ofisi ya spika kabla ya kwenda kutoa taarifa kwa vyombo vya habari.

Alipoulizwa kuhusu hatua atakayoichukua baada ya kupokea barua ya Nyalandu, Ndugai alisema kwamba, kwa sasa hawezi kuzungumzia kitu ambacho hakijatokea, lakini endapo atapokea barua hiyo, na Nyalandu akathibitisha kwamba ni ya kwake, basi wataweza kukaa kujadili uamuzi huo.

Katika taarifa yake ya asubuhi, Nyalandu alisema kuwa, amemuandikia Spika Ndugai barua ya kujiuzulu Ubunge ambao ameutumikia tangu mwaka 2000.

“…asubuhi ya leo nimemwandikia Spika wa Bunge, Mh. Job Ndugai, Mb., barua ya kujiuzulu nafasi yangu ya UBUNGE wa Jimbo la Singida Kaskazini kupitia tiketi ya CCM, nafasi ambayo nimeitumikia kwa vipindi vinne mfululizo tangu nilipochaguliwa kwa mara ya kwanza mnamo mwaka 2000 hadi Sasa.”

chanzo: zanzibar24.

Comments