Moto uliowashwa na Mama wamteketeza Mwana Tanga.

Mtoto wa miaka 3 ameungua na moto hadi kufa moto ambao uliwashwa na mama yake mzazi wakati wakiwa shambani kwa lengo la kupikia.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tanga RPC Benedict Michael Wakulyamba amethibitisha tukio hilo lililotokea  Oktoba 12 mwaka huu katika kijiji cha Kwamwenda Kata ya Mlorwa Wilaya ya Handeni mkoani Tanga ambapo mtoto Kessy Kamuje mwenye miaka 3 amefariki kwa kuungua moto akiwa shambani na mama yake mzazi.


“Ni kweli tukio limetokea jana ambapo mtoto Kessy aliungua kwa moto baada ya mama yake kumlaza kwenye kibanda cha nyasi shambani ambacho kilishika moto aliokuwa ameuwasha kwaajili ya kupikia”,amesema RPC Benedict.

Kamanda ameeleza kuwa mama wa mtoto Kessy alifika shambani kwaajili ya shughuli za kilimo ambapo alimlaza mtoto kwenye kibanda cha nyasi na akawasha moto kwaajili ya kupika kisha akaendelea na shughuli za kilimo ndipo Kibanda kikashika moto na kumuunguza hadi kufa mtoto Kessy.

chanzo: zanzibar24.

Comments