
Hayo yalisemwa na wanafunzi mbali mbali kutoka katika skuli
sita kutoka Mjini na Magharibi B wakati walipofanya mdahalo
unaohusiana na utandawazi huko katika ukumbi wa sanaa Rahaleo Mjini
hapa.
Walisema matumizi mabaya ya mitandao kwa wanafunzi kwa kuangalia
picha zisizokuwa na maadili ni miongoni mwa mambo yanayowasababishia
baaadhi ya wanafunzi kujiingiza katika vishawishi vibaya.
Mmoja wa wanafunzi hao Ismail Mohamed Awadh kutoka skuli ya mtopepo
alisema baadhi ya wazee huwa ni chanzo cha kupotea maadili kwa wanafunzi
kutokana na kununuliwa simu ambazo hazikustahiki kuwa nazo kwa wakiti
huo.
“Kundi kubwa la wanafunzi ambalo linaathirika katika masuala ya
maadili ni wale wanaotumia mitandao ya kijamii kwa muda mrefu, ila hili
linatokana na wanafunzi hao kununuliwa simu hizo na wazazi wao”alisema
Awadhi.
Aliongeza kusema kuwa “lakini pia simu hizo baadhi ya wakati huwa ni
chanzo cha wanafunzi kupata mimba katikia umri mdogo tena akiwa bado ni
mwanafunzi”.
Fatma Abdallah kutoka skuli ya Haile Selasie alisema kuwa matumizi ya
simu yasiofuta taratibu nzuri kwa wanafunzi pia kunachangia wanafunzi
kuiga tamaduni za nchi zilizoendelea.
Alitoa mfanowa hayo kwa kusema kuwa “Utawakuta wanafunzio wanavaa
kama walivyo watu wan je ya Zanzibar, huku wakieka kando taamaduni na
silka zao wakichangiwa na matumizi ya mitandao ya kijamii”alisema.
Hata hivyo alisema kuwa suala la uvivu kwa wanafunzi katika masomo
yao nalo linachangiwa na matumizi mabaya ya utandawazi, hali ambayo mara
nyingi huchangiwa kwa kuwepo mashine mbali mbali za kufanyia kazi hasa
za nyumbani ikiwemo kupikia kufulia na kadhalika .
Wanafunzi hao walisema kuwa pamoja na kwuepo kwa hali hiyo lakini
bado matumizi ya mitandao ina faida pindi mtumiaji akiitumia
kwa maslahi ya kujiongezea elimu au kutafuta taarifa za maendeleo.
Nae Mwalimu wa Skuli ya Sekondari Fuoni, Fatma Ali alisema mada
iliowasilishwa ni nzuri ambayo imo katika masomo ya Civics na English
hatua ambayo inaweza kuwasaidia kutoa mbinu tofauti kwa wanafunzi hao
kutokana na uwasilishwaji wa wenzao.
Ali alitoa wito kwa wazee kutoa mashirikiano na walimu katika
maendeleo ya wanafunzi pamoja na utaratibu mzima wa ulezi kwa wanafunzi
ili waweze kuepukana na vitendo vya udhalilishaji kwa wanafunzi hao.
Nae Msaidizi mratibu wa mfuko wa kusaidia watoto Mariyam Jecha
Salum alisema lengo la mradi ni kuinua ufahamu na uimarishaji kwa
viongozi wa mabaraza ya skuli yanahusiana na uhifadhi wa mtoto pamoja
na kutoa elimu ya stadi za maisha ,kutumia vipaji na mengineo.
Skuli ambazo zilishiriki katika mdahalo huo ni Skuli ya Haile-
Sallassie Mwembeshauri ,Rahaleo kwa wilaya ya mjini na magharibi ni
Fuoni, Mtopepo B na Mwanakherekwe kongamano hilo limefadhiliwa na Mfuko
wa kusaidia watoto (Global Fund for Children) kushirikiana na Jumuiya ya
wanasheria Wanawake Zanzibar ( ZAFELA .)
chanzo:zanzibar24.
Comments