Mahakama ya vileo z’bar yawafungia mkanda wamiliki wa baa.

Mahakama ya Vileo Zanzibar  imesema  haita sita kuzifungia baa zilizokosa vigenzo  vya  kufanyabiashara pamoja na zile zinazoleta usumbufu  katika makaazi ya wananchi na zile zilofungiwa na  bado  zikaendelea kufanya biashara.

Akizungumza na Zanzibar24 katika ziara ya ukaguzi wa baa za Magharibi “A” Katibu wa Mahakama hiyo Saleh Ali Abdallah amesema  kuna baa bado zinapinga  maagizo yaliyotolewa na mahakama  hasa katika suala la usafi wa afya katika maeneo ya biashara hizo jambo ambalo litaweza kuhatarisha afya za wateja.


Hata hivyo  amesema  kuna baadhi ya baa  hizo  zipo karibu na makaazi ya wananchi  na nyengine zipo karibu na nyumba za ibada  hatua kali zitachukuliwa  kwa  watakao  epuka sheria zilizowekwa.

Zaidi ya baa Ishirini na 8 zimefanyiwa ukaguzi na Mahakama ya vileo Zanzibar  katika Wilaya ya Magharib “A” na  kutoa wito kwa wananchi kuwacha  tabia ya kulalamika pembeni badala yake  kupeleka malalamiko yao sehemu husika ili kupatiwa ufumbuzi.
chanzo: zanzibar24.

Comments