
Wakizungumza mara baada ya kufungua Akaunti wasizozitarajia kwenye
bonde la kilimo Mtakata baadhi ya wakulima wa mbogamboga wamesema
hawakuwa na ubishi walipo waona maafisa wa bank ya CRDB wakiingia
kondeni ingawa walipo waona walidhani ni viongozi wa serikali wanakuja
kuwakagua hivyo walijawa na furaha walipo ona kumbe ni maafisa wa bank
kwani wamepata huduma pasi kupoteza muda wala nauli.
Meneja wa CRDB Ahmed Abuubakar amesema wameamua kwenda kuwafungulia
akaunti wakulima kwenye konde kwa kujali muda wao huku bank ikijipanga
kuwakopesha wakulima hao wazalishe zaidi, mikopo itakayo kuzingatia
taratibu za milazao bila ya kuwa na riba ilikukuza kilimo kisiwani
Pemba.
Afisa kilimo kutoka wizara ya kilimo maliasili mifugo na uvuvi Ali
Said Yusufu amesema kufika kwa bank hio kutoa mashirikiano kutasaidia
kuwawezesha wakulima Pemba kutatua changamoto zinazowakabili kutokana na
ukosefu wa fedha.
chanzo: zanzibar24.
Comments