Kiongozi wa CHADEMA aendelea kusota rumande.

Mkurugenzi wa Operasheni na mafunzo wa CHADEMA Benson Kigaila, ambaye ameshikiliwa na polisi jana kwa tuhuma za kutoa lugha zinazodaiwa kuwa za kichochezi bado ameendelea kusota rumande mpaka sasa kwani dhamna yake bado haijatolewa.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum Lazaro Mambosasa, amethibitisha kuwepo kwa Kigaila rumande katika kituo kikuu cha polisi kanda maalum, na kusema kwamba bado wanamshikilia Kigaila mpaka pale uchunguzi utakapokamilika na kumpa dhamana, na hatimaye kufikishwa mahakamani kujibu tuhuma zinazomkabili.


“Kigaila bado tunaye dhamana yake bado hajapata, tunaendelea na uchunguzi tukijiridhisha tutampa dhamna na kumpeleka mahakamani kujibu mashtaka yake”, amesema Mambosasa.

Bw. Kigaila anashiikiliwa kwa tuhuma za kutoa lugha za kichochezi Oktoba 12 katika mkutano wake na waandishi wa habari.

Chanzo: zanzibar24.

Comments