
Kamishna Jenerali Malewa ameyasema hayo wakati akiwa kwenye ziara
huko mkoa wa Pwani kwa lengo la kukagua miundombinu katika gereza la
mahabusu la Mkuza,picha ya ndege, gereza la Kigongili wilayani Bagamoyo
na kuweka jiwe la msingi katika gereza la Mkuza.
“Pamoja na changamoto nyingi ambazo nimezikuta changamoto
kubwa ni makazi ya askari nyumba za askari hazitoshi zilizokuwepo
zimechakaa zingine zinahitaji ukarabati mkubwa tu, nimekuja kujionea
mwenyewe hali halisi ilivyo ili nikirudi ofisini nione tunafanyaje ili
tuweze kusaidia angalau kukarabati ili ziwe katika hali nzuri,lakini
kubwa tunalolitaka kwa askari wetu nikutumia rasilimali zilizopo katika
vituo vyao vizuri,” alisema Kamishna Jenerali Malewa.
Aidha alikutana na Mkuu wa Mkoa wa Pwani, Mhandisi Evaristi Ndikilo
ambapo mbali na kuzungumzia makazi duni ya askari, Mkuu wa mkoa huyo
amemuomba Jenerali Malewa kuangalia namna ya kuboresha maslahi kwa
watumishi wake.
chanzo: zanzibar24.
Comments