
Kamanda wa Polisi Mkoani humo, Shehan Mohamed Shehan, alisema kijana
huyo, alitoroka baada ya kushitukia kuwa anafautwa na Polisi, baada ya
kufanya kosa hilo.
Alisema kijana huyo alikwenda kijiji cha Makombeni Oktoba 23, na
alipofika, alimtorosha msichana huyo na kumpeleka Changaweni kwa lengo
la kumingilia.
Alisema baada ya mtoto huyo kuhojiwa, ndipo taarifa zilipowafikia na
kuanza kumtafuta, ingawa taarifa za awali zilionyesha amekimbia.
“Jeshi ka Polisi linamtafuta kila kona, na limeshaweka mitego, ili
kuhakikisha anapatikana na kufika mbele ya mkono wa sheria
kujieleza”,alisema.
Hata hivyo amewataka wazazi na walezi, kuwa karibu na watoto wao, na
kila baada ya muda kujua walipo, ili kuweza kutatua changamoto kama hizo
zinapowatokea.
chanzo: zanzibar24.
Comments