Acharazwa mapanga kwatuhuma ya kuiba ng’ombe Unguja.

Tukio hilo limetokea hapo juzi majira ya saa 10 hadi saa 11 alfajiri ambapo kijana aliefahamika kwa jina la Hamadi Rashid ambae alikuwa anatoka kwenyestarehe huko Mbejuu, hatimae alipofika Unguja Ukuu Kaibona alipigwa mapanga na vijana wasiojulikana kwa madai yakuwa anataka kuiba ngombe.

Kwa mujibu wa taarifa kutoka kwa kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Unguja Juma Sadi Khamisi amesema kuwa  katika utafiti wanaoufanya mpaka sasa wameweza kupata jina la mtuhumiwa mmoja ambae wanamtafuta na ambapo watafanikiwa kumpata itakuwa njia sashihi ya kuweza kuwapata na wahusika wengine.


Hata hivyo Kamanda Sadi ameifahamisha jamii kutochukua hatua mikononi mwao nakuacha tabia kama hiyo na watahakikisha waliofanya kitendo hicho watakamatwa na watafikishwa kwenye vyombo husika.

Baba wa mtoto  huyo amefunguka kwa kusema kuwa “mwanangu wamempiga mapanga sisi tulipopata taarifa tulimpeleka kituwoni nakamakawaida tukapewa ruhusa ya kuenda Hospitali, hali yake ni  mbaya kwani wamem`chinja mkono, miguu, alimradi wamemchinja vibaya vibaya.”

Hivi sasa Kijana Hamadi yupo katika Hospitali ya Mnazimmoja na hali yake sio nzuri.
chanzo:zanzibar24.

Comments