
Wakizungumza katika mkutano wa siku nne unao fanyika kwenye ukumbi wa
Hoteli ya Pemba Misali Wesha nje kidogo ya mji wa Chake chake
Mwakilishi wa Shirika la afya ulimwenguni WHO Dr Alphoncia Nanai
alisema shirika lake lina lengo la kutokomeza magonjwa 17 yasio pewa
kipao mbele ikiwemo kichocho mkakati ambao umelenga ifikapo 2020 uwe
umekamiika.
Alisema kwa mujibu wa utafiti ulio fanywa ugonjwa wa kicho cho
unaweza ukamalizika kabisa pindi wakitokomeza mdudu konokono anae ishi
kwenye maji ambae ndie anae zalisha wadudu wanao ambukiza ugonjwa wa
kicho cho.
Alisema huo nimkutano muhimu wenye lengo la kujenga uwezo kwa nchi
nane barani afrika ikiwemo tanzania ilikudhipiti waduduhao wanao pia
kwenye ngozi na kuingia kwenye kibofu cha mkonjo kutoka kwa mdudu
konokono.
Hivyo wameamua kutoa mafunzo ya namna ya kumtokomeza mdudu huyo
konokono kwani hata wakitoa dawa kwa mgonjwa hupona ila anarejea tena
kwenye maji naakakutana tena na mdudu huyo hupata tena magonjwa hivyo
njia ya kudhibiti ugonjwa huo nikumuuwa kapisa konokono.
Kwa upndewake Dr paulin mwenzi wa shirika hilo kwa upande wa Kenya
alizitaja nchi zilizo shiriki mkutano huo kuwa ni Kenya .Ithopia, Gana,
Uganda, Mozampiq, Ruwanda, Tanzania na wenyeji Zanzibar
Alisema sababu ya kuchaguliwa Zanzibar kuwa nisehemu ya majaribio kwa
bara la afrika nikutokana utafiti ulio onyesha kuwa kichocho kimepungua
sana hasa Pemba ambapo kama wakitokomeza vyanzo sababishi nidhahiri
uwezekano wa kumaliza ugonjwa huo utapatikana.
Mkuu wa maabara ya Jamii kisiwani Pemba alisema licha ya kuwa kisiwa
cha Pemba kinakabiliwa na maeneo mengi yenye maji kama haya ya baridi
ambapo mdudu huyu konokono yupo na watu hasa watoto wana tumia sana
ila utafiti wao umeonyesha uwepo uwezekano wa mafanikio ya kumaliza
ugonjwahuo wa kichocho kwasasa ulivyo pungua
Alisema wanaelewa kuwa Pemnba inamaeneo mengi ya mabwawa ya maji
yanayo tumiwa na watu na inavyanzo vingi ila wamekusudia Pemba kwavile
mapitio ya awali yalionyesha kuwa asilimia 8 ya watu wanaugonjwa ila
baada ya kufanya matibabu sasa ni alsilimia mbili tu.
Mtaalamu kutoka nchini china Dr chenqeen chaciin amesema uzoefu walio
pata kutoka china nikuwa dawa watakayo tumia kisiwani pemba nidawa
salama kwa binaadamu baada ya siku tatu kuingizwa kwenye maji kuuwa
vimelea vilivyomo kwenye konokono watu wanaweza kutumia maji hayo
yakiwasalama bila ya madhara yoyote.
chanzo:zanzibar24.
Comments