
Akithibitisha hilo Sheha wa Shehia ya pangawe Abdallah Juma Mtumweni
amesema katika kupambana na zoezi hilo kwa kushirikiana na Wizara ya
Afya kesho wanatarajia kuendesha zoezi la chanjo na kuwaomba wenye
wanyama hao kutumia fufsa hiyo.
“Serikali kwa makusudi ilikuwajali wananchi wake wameamua
kutoa tena chanjo hizi za maradhi dhidi ya kichaa cha mbwa, kwaiyo
nawaomba wanajamii nawaomba ten asana wajitokeze kwa wingi kila mwenye
mbwa awalete ili kupatiwa chanjo hii kwani chanjo hii inayotolewa ni
inaleta manufaa kwetu sote sio watoto tu bali hata watu wazima kwani
mbwa kichaa hachagui rika yoyote ya kumg’ata binadamu”
Kwa upande wake mkaazi wa eneo hilo Issa Muhammed Zonga amefahamisha
kuwa athari ya kichaa cha mbwa ni kubwa ikiwemo gharama na hata
kusababisha kifo.
“ homa ya kichaa cha mbwa ni homa mbaya sana kwasababu
unapokosa huduma mapema hatimayake husababisha kifo. Kwakweli nawambia
wanaofuga mbwa na hata paka wasidharau kuwapeleka Hospitali kusubiri
kwamba mpaka wapate athari ya maradhi na baadae kupita mitaani kuathiri
wananchi, Siku wanayosikia kuwa madaktari wanakuja kwaajili ya wanyama
wapeleke wanyama wao kwenda kupiga sindano kwa usalama wa wananchi”.
chanzo: zanzibar24.
Comments