SMZ yatakiwa kuchunguza kwa makinimiradi ya TASAF.

Kamati ya kusimamia ofisi ya Viongozi  Wakuu wa kitaifa katika Baraza la wawakilishi imesema haijaridhishwa na  Uekezaji wa miradi ya kusaidia kaya masikini TASAF kutokana na miradi hiyo kushindwa kuendelezwa baada ya kukamilika.

Akisoma hutuba ya kamati hiyo katika kikao cha Baraza la wawakilishi chukwani nnje kidogo ya mji wa Zanzibar Mwenyekiti wa kamati hiyo  Omar Seif Abeid amesema licha ya serikali kuwa na utaratibu wa kuwasidia kaya masikini lakini kaya hizo zimekuwa  hazinufaiki na miradi hiyo kutokana na kushindwa kusimamiwa.


Aidha ametowa wito kwa taasisi zinazosimamia mradi wa kaya masikini TASAF kufanya kazi kwa bidii ili wananchi waweze kunufaika na maradi huo katika kujikwamua kiuchumi..

Akijibu hoja za wajumbe wa baraza la wawakilishi, Waziri wa nchi ofisi ya makamo wa pili wa rais Mohamed Aboud Mohamed amesema kutokana na fedha nyingi kutumika kwa ajili ya kuendeleza miradi hiyo serikali itaendelea kuzikumbusha taasisi husika ziendelee kuisimamia na kuiendeleza ili iweze kuwanufaisha wananchi.

Hata hivyo amesema zaidi ya kaya mia 3 hapa Zanzibar zimepoteza sifa za kuendelea na TASSAF kutokana na matukio mbali mbali ikwemo wananchi kuhama makaazi yao na wengine kupoteza maisha.
chanzo:zanzibar24.

Comments