
Katika mkutano huo shughuli mbali mbali zinatarajiwa kufanyika ambapo jumla ya maswali 136 yataulizwa na kujibiwa.
Hayo yalielezwa na Katibu wa Baraza la Wawakilishi, Raya Issa Mselem,
alipokuwa akitoa taarifa ya shughuli za mkutano huo kwa waandishi wa
habari jana.
Alisema katika kikao hicho kutakuwa na miswada miwili ya sheria
ambayo iliwasilishwa na kusomwa kwa mara ya kwanza katika mkutano wa
Mei-Juni, 2017 ambayo itasomwa kwa mara ya pili na kujadiliwa.
Alitaja miswada hiyo kuwa ni muswada wa sheria ya kufuta sheria ya
mahakama ya kadhi namba 3 ya 1985 na kuanzisha upya mahakama ya kadhi na
kuweka masharti mengine yanayohusiana na hayo.
Alisema muswada mwengine ni wa sheria ya kuanzisha Baraza la Taifa la Biashara na kuweka mambo mengine yanayohusiana na hayo.
Pia alisema shughuli nyengine ambazo zimekusudiwa kutekelezwa katika
mkutano huo ni kuwasilishwa ripoti za Wizara za SMZ kuhusu utekelezaji
wa maagizo ya kamati za kudumu za Baraza.
Aidha alisema shughuli nyengine ni na kupokea taarifa ya serikali
kuhusu ripoti ya utekelezaji wa mamlaka ya maji Zanzibar (ZAWA) na
miswaada mengine itakayosomwa kwa mara ya kwanza.
chanzo: zanzibar24.
Comments