Marekani imeeleza kusikitishwa na tukio la kushambuliwa kwa risasi Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu.
“Tunalaani
kitendo hiki cha kipuuzi na cha kutumia nguvu,” imesema taarifa ya
Ubalozi wa Marekani nchini iliyotolewa kupitia ukurasa wake wa Facebook.
Ubalozi
huo umesema unaungana na Watanzania katika kumtakia kheri Lissu ambaye
pia ni Rais wa Chama cha Wanasheria wa Tanganyika (TLS) ili apone
haraka.
Lissu jana Alhamisi saa sita usiku alisafirishwa kwa matibabu katika Hospitali ya Aga Khan iliyopo Nairobi, Kenya.
Awali, alipatiwa matibabu katika Hospitali ya Rufaa ya Dodoma baada ya kushambuliwa.
Spika
wa Bunge, Job Ndugai amesema leo Ijumaa asubuhi kuwa, Lissu
alishambuliwa kwa risasi kati ya 28 hadi 32, huku tano zikimpata
mwilini.
Akitoa
taarifa ya tukio hilo kwenye kikao cha Bunge, Ndugai amesema risasi
mbili zilimpata Lissu kwenye miguu, mbili tumboni na moja kwenye mkono.
chanzo:Mpekuziblog.
Comments