Ipo haja ya kujirejea Utamaduni wa kizamani Dkt. Fadhil.

Mkurugenzi wa Kinga na Elimu ya Afya Dkt. Fadhil Mo’hd Abdalla amesema iko haja kurejea utaratibu  wa kizamani , wataalamu wa afya ya kinywa na meno kutoa huduma za matibabu katika maeneo mbali mbali ikiwemo maeneo ya maskuli na vijijini .

Hayo aliyaeleza katika Kituo cha Afya Rahaleo, wakati akifungua zoezi la uchunguzi wa afya ya kinywa na meno linaloendeshwa na Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno kutoka Tanzania .

Alisema afya hiyo ni muhimu kufanyika awali kabla ya madhara, kwa kupatiwa ushauri wa mapema kabla ya athari kujitokeza na kusababishwa kupoteza meno .
Alifahamisha kuwa katika miaka ya nyuma elimu ya afya ya kinywa na meno zilikuwa zikitolewa katika maskuli ,wataalamu hutoa  elimu kwa wanafunzi pamoja na kung’oa meno kwa  wale ambao meno yao yameadhirika .
“Huu usiwe  mwanzo  wa kuonyesha njia kwa jamii na wala msisubiri kuumwa kila muda mujiwekee utaratibu wa kujichunguza afya zenu ikiwemo afya ya kinywa na meno pamoja na maradhi yasioambukiza ili muweze kupata ushauri mapema kwa Madaktari ,”alisema Mkurugenzi Kinga  .
Alieleza kutoa  elimu na uchunguzi wa afya  kwa jamii itasaidia kupunguza gharama za matibabu  na kuimarisha  kinga ya awali na kujiepusha na matumizi ya vyakula ambavyo vinachangia kuleta madhara ikiwemo vyakula vya sukari  kuchangia uozeshaji wa  meno hasa kwa watoto .
Nae Mwenyekiti wa Chama cha Madaktari wa Afya ya Kinywa na Meno ( TBA) Dkt Lorna Carneiro  alisema mara hii wamepata fursa ya kuja Zanzibar kwa kufanya uchunguzi wa afya ya kinywa na meno ili kujua wale wagonjwa  ambao wanamatatizo na kuwapatia tiba pamoja  na kuwapa  elimu ya afya .
Alisema Chama hicho  kinahimiza umuhimu  wa afya bora kwa jamii na kutoa ushauri wa maradhi mbalimbali ikiwemo ukimwi ,saratani ,Kifua kikuu,afya ya kinywa na meno pamoja na maradhi yasioambukiza  kwa kuifanya jamii ipate uelewa  na kujikinga na maradhi ambayo yanauwezo wa kuepukika .
“Hali ya idadi ya  Wagonjwa ni kubwa wakati ya kuwa magonjwa haya yanakingika kwa haraka na kupona lakini kikwazo ni kuwa na uchache wa madaktari ,“alisema Dr Lorna .
Alifahamisha kila ifikapo tarehe 20  machi ya kila mwaka huadhimisha siku ya afya ya kinywa na meno kwa mwaka ujao wanatarajia uzinduzi  wa zoezi hilo litafanyika Zanzibar .
Nae Mgonjwa BI Nargisi Uzia ambae alifika kupatiwa huduma ya matibabu katika kituo hicho alisema anaishukuru Serikali kwa kuwaletea wataalamu wa kuchunguza afya zao lakini pia iko haja ya zoezi hilo liwe endelevu kwani matatizo yako mengi yanahitaji uchunguzi.
Rais wa Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania Dkt.Lorna Carneiro kulia  akitoa hotuba ya makaribisho katikaUfunguzi wa  Zoezi la Uchunguzi wa Maradhi ya kinywa na Meno katika Kituo cha Afya Rahaleo Mjini Unguja.

Mkurugenzi wa Kinga na Elimu ya Afya katika Hospitali ya Mnazi mmoja Dkt,Fadhil Abdalla akitoa hotuba ya Ufunguzi wa Zoezi la Uchunguzi wa  Maradhi ya Kinywa na Meno  katika Kituo cha Afya Rahaleo Mjini Unguja.Zoezi linalofanywa na Chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania(TDA).wakishirikiana na madaktari wa Zanzibar.
Mkurugenzi wa Kinga na Elimu ya Afya katika Hospitali ya Mnazi mmoja Dkt,Fadhil Abdalla katikati akiwa katika picha ya pamoja na Madaktari kutoka Chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania(TDA).pamoja na madaktari wa Zanzibar katika  Zoezi la Uchunguzi wa  Maradhi ya Kinywa na Meno  katika Kituo cha Afya Rahaleo Mjini Unguja.
Rais wa Chama cha Madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania Dkt,Lorna Carneiro kushoto akifanya mahojiano na Muandishi wa Habari kutoka ITV Farouk Kariym pamoja na  muandishi wa Habari Maelezo Zanzibar Khadija Khamis katika  Ufunguzi wa Zoezi la Uchunguzi wa  Maradhi ya Kinywa na Meno  katika Kituo cha Afya Rahaleo Mjini Unguja.Zoezi linalofanywa na Chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania(TDA).wakishirikiana na madaktari wa Zanzibar.
Daktari wa Kinywa na Meno kutoka Haspitali ya Arrahma Zanzibar akimfanyia Uchunguzi wa  maradhi ya Kinywa na Meno Kauthar Vuai mkaazi wa meli nne, katika Zoezi la Uchunguzi wa  Maradhi ya Kinywa na Meno  katika Kituo cha Afya Rahaleo Mjini Unguja.Zoezi linalofanywa na Chama cha madaktari wa Kinywa na Meno Tanzania(TDA).wakishirikiana na madaktari wa Zanzibar.
chanzo:Zanzibar24

Comments