Ilivyo jipanaga SMZ kupabmana na dawa zakulevya 2017.

wawakilishiSerikali ya Mapinduzi Zanzibar imeongeza zaidi ya shiling milioni miatano tisini  na nane  katika bajeti ya mwaka wa fedha 2017 hadi 2018 ili kupambana na madawa ya kulevya  nchini.

Akitoa taarifa juu ya utekelezaji wa maagizo ya kamati ya kudumu ya baraza la wawakilishi ya kusimamia ofisi za viongozi wakuu wa kitaifa kwa mwaka wa fedha 2017 hadi 2018 Waziri wanchi Ofisi ya Makamo wa Pili wa Rais Mohammed Aboud Mohammed amesema ongezeko hilo ni la  asilimia 36 ulikinganisha na bajeti ya mwaka wa fedha 2016 hadi 2017 ambapo zaidi ya shiling milioni mianne na salasini na sita zilitolewa kwa ajili ya  shughuli hizo zimelenga kupambana na janga hilo.


Amesema kuwa serikali imeamua kuongeza bajeti hiyo ili kufikia lengo la kudhibiti uingizwaji  na usafirishaji wa dawa za kulevya nchini pamoja na kukabiliana na matatizo yanayojitokeza katika uendeshaji wa kazi hizo.

Kwaupande wao baadhi ya Wajumbe Akiwemo Soud  Said Soud na Riziki Pembe Juma Wakizungumza na Zanzibar24 mara baada ya kuwasilisha kwa Ripoti hiyo  wametoa maoni yao juu ya kutafuta  mikakati imara ya kukomesha  uingizaji na ushambazaji wa madawa ya kulevya nchini.

Wamesema  endapo sheria zilizopo zitatumika  bila ya muhali  itasaidia  kwa kiasi kikubwa  kupamba na  kuwakamata  wahalifu wa madawa ya kulevya nchini.

Aidha wametoa wito katika jamii  kutoa ushirikiano kwa serikali katika  kuwafichua  wauzaji na wasambazaji wa madawa ya kulevya kwani serikali imejipanga  kuwatia nguvuni  na  kuwafikisha katika vyombo vya sheria.

chanzo:

Comments