
IGP Sirro ameyasema hayo leo alipokuwa akizungumza na waandishi wa
habari na kudai usalama wa nchi upo vizuri na jeshi la polisi limeongeza
nguvu ya upelelezi mjini Dodoma ili kuhakikisha linawapata watu ambao
wamefanya uhalifu wa kumpiga risasi mbunge Tundu Lissu , huku akiwataka
wananchi wasihusishe tukio hilo na masuala ya kisiasa.
“Naomba wananchi wasidanganywe kwenye suala zima la siasa
na vitu vingine hapa huwa nasema siku zote kama hakuna amani na usalama
siasa haiwezi kupata nafasi ili tukio limetokea tunapeleleza na tupo
makini na hili tukio, kwa sasa tumeongeza vikosi vya upelelezi Dodoma,
wale waliofanya lile tukio ni lazima tutawakamata ila upelelezi huu
unaweza kuzaa matunda mazuri zaidi endapo wananchi watatupa ushirikiano
wa kutosha” alisema IGP Sirro.
Aidha IGP Sirro amezungumzia moja ya kauli ya Tundu Lissu aliyowahi kuisema kuwa “kuna watu wananifuatilia”
na kuvitaka vyombo vya usalama kuacha kuwatuma watu hao kumfuatilia na
kudai kuwa hakuwahi kuripoti katika kituo chochote cha polisi, na kusema
sasa usiwe wakati wa kuzungumzia jambo hilo.
IGP Sirro alimalizia kwa kusema kuwa jeshi la polisi lipo imara na lipo kwa ajili ya kulinda watanzania pamoja na mali zao.
chanzo: zanzibar24.
Comments