
Baada ya kumkamata kijana huyo siku ya Ijumaa na kumfikisha
mahakamani siku ya Jumatatu, polisi wameeleza kuwa Andrwer alimpiga
risasi moja ya kichwa mama yake huyo aliyekutwa akiwa kitandani baada ya
kumtupa nje mtoto wa mbwa aliyompeleka nyumbani kwao.
Licha ya kuwa mahakama ilimkuta kijana huyo na kosa la mauaji ila,
polisi wamedai kuwa walipokea simu majira ya asubuhi kutoka kwa kijana
huyo akidai kuwa amerudi nyumbani na amemkuta mama ameuwawa.
Akitoa ushahidi mahakanani mpelelezi wa makosa Charles Buckland,
amesemea kuwa ni kijana huyo na mama ndiyo walikuwa nyumbani usiku wa
tukio. ” Andrew Willson aliongea na mama usiku wa Alhamisi kuhusiana na kumpeleka mbwa huyo kwa baba yake,” amesma mpelelezi.
Akaongeza kuwa “Ilipofika usiku wa manane kijana huyo
alichukua bunduki yenye risasi 22 na akaenda chumbani kwa mama yake
akafyatulia kichwani wakati mama yake huyo akiwa amelala.”
Chanzo: USA Today:zanzibar24.
Comments