Akizungumza
na waandishi wa habari ofisini kwake Chake chake Pemba Mdhamin wa Mamlaka hiyo Pemba
Nd. Suleiman Ame Juma amesema mtuhumiwa
huyo amedaiwa kuomba rushwa hiyo kwa mtu ambae jina lake lime hifadhiwa kwa
kosa la kuwekewa zuiyo la kuto endelea na ujenzi katika eneo la Gombani kKisiwani
Pemba.
Amesema kuwa
mtuhumiwa huyo amepatikana na tuhma hizo baada ya kuskiliza malalamiko
nakuandaa mtego maalum waliomnsa wakati akipokea fedha ambazio sio halali kwake
kutoka kwa mlalamikaji huko ofisini kwake Machomanne siku ya jumatatu ya tarehe
31/7/2017 baada ya kupokea kiwa hicho cha fedha alicho akinadai endapo
atapatiwa atamuwezesha kuendeleza na ujenzi wake ulio sitishwa.
Aidha
amefahamisha kuwa sivyema kwa viongozi wa taasisi na idara mbali mbali kutumia
vyeo vyao vibaya kwa kuwakandamiza walio chini kwani kufanya hivyo nikosa
kisheria nao kama mamlaka husika wakilibalia watamuajibisha muhusika wa tendo
hilo.
Hatahivyo
amesema kuwa hilo nitukio la pili ndani ya mwezi uliopita na sasa waendelea na
uchunguzi juu ya mtendaji huyo na endapo ushahidi utakamilika watamfikisha
mahakani ilikujibu shutma zinazo mkabili dhidi yake ikiwa kwa sasa yupo nje kwa
dhamana.
ZAECA imekuwa
ikiyachukulia hatua matuo yote ya rushwa na uhujumu uchumi kwa watendaji
mbalimbali wanao hisika na kuomba rushwa kwa kujinufaisha wao wenyewe na
matumbo yao hivyo kuahidi kuzi tafutia ufumbuzi kero hizo.
Comments