Uuzaji na Ununuzi Karafuu kiholelela wapigwa marufuku Pemba.

Mkuu wa wilaya  ya wete Rashid Hadidi Rashid amesema  si ruhusa kwa Mwananchi yoyote kununua ama kuuza karafuu kwa njia ya kikombe na atakae kwenda  kinyume hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi yao.
Kauli hiyo ameitoa wakati alipokuwa akizungumza na wanunuzi  ama  wauzaji  wa karafuu kwa njia ya kikombe huko ofisini kwake wete.

Amesema ununuzi wa karafuu kwa njia ya vikombe kunachangia wizi wa karafuu hivyo ameeleza kuwa mtu yoyote ambae  atakamatwa akinunua ama kuuza  karafuu hatua  za  kisheria zituchukuliwa dhidi yao.
Aidha mkuu huyo wa wilaya amewataka wananchi kutouza karafuu zao majumbani na badala yake waziuze karafuu zao  katika vituo  vya ZSTC ili serekali iweze kujipatia mapato kupitia  zao  hilo.
Na OCD wilaya ya wete Hamad Omar Sleiman amesema kumejitokeza baadhi ya watu huchukua karafuu kutoka tanga kwa njia ya magendo na kuzichanganya na karafuu za pemba jambo ambalo linapelekea karafuu za pemba kuzipotezea sifa yake hivyo mtu yoyote atakae kamatwa hatua za kisheria  zitachukuliwa.
Kwa upande  wa Wananchi  wameahidi  kushirikiana na ofisi ya mkuu wa wilaya  na kuhakikisha  kwamba  wanaufikisha  ujumbe huo kwa wananchi wengine.
 chanzo:zanzibar24.

Comments