SMZ yazindua mpango kazi utakaorudisha heshima ya wanawake na watoto Zanzibar.

Rais  wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dr.Ali Mohamed Shein amesema mpango  kazi wa kitaifa wa kumaliza  ukatili na udhalilishaji Zanzibar  ni azma ya serikali  ya mda mrefu yakutaka kuirejesha hadhi ya mwanamke na mtoto katika jamii.

Waziri wa kazi Uwezeshaji,wazee,vijana,wanawake na watoto Maudline Cyrus Castico akitembelea maonyesho mbalimbali yaliyoandaliwa na asasi za kiraia kudhibiti vitendo vya ukatili naudhalilishaji wanawake na watoto Zanzibar..
Akizindua mpango huo kwa niaba ya Rais wa Zanzibar  Waziri wa kazi Uwezeshaji,wazee,vijana,wanawake na watoto Maudline Cyrus Castico  amesema Serikali  ya Mapinduzi Zanzibar imezindua mpango kazi huo  utakaofanyakazi kwa muda wa  miaka mitano, utategemea kumaliza  ukatili na udhalilishaji dhidi ya wanawake  na watoto  Zanzibar.
Amesema mpango huo umeweka  mikakati imara ya  kuvidhibiti vitendo vya ukatili na udhalilishaji visiweze kutokea Zanzibar na endapo vikitokea  mpango huo uweze kufanya kazi kiuadilifu.
Wakuu wa mikoa pamoja na wakuu wa wilaya na viongozi mbalimbali wakifuatilia maadhimisho ya mpango kazi wa kudhibiti vitendo vya ukatili na udhalilishaji wanawake na watoto Zanzibar.
Kwaupande  wake mtoto  Jaffar Ahmada akisoma risala kwa niaba ya watoto wa Zanzibar  amesema vitendo  vya ukatili na udhalilishaji wanavyofanyiwa na jamiii inayowazunguka vimekuwa vinawarudisha nyuma na kuwaumiza kisaikolojia kama vile kupigwa,kulawitia,kuchomwamoto pamoja na vichanga kutupwa.
Aidha wameitaka serikali kwa kushirikiana na mashirika ya kimataifa pamoja na wadau wa maendeleo  nchini  kuchukua hatua madhubuti  zitakazotumika katika  mpango huo wa miaka mitano kutoa adhabu kali  kwa wataohusika  na  vitendo vya kuwadhalilisha watoto.
Wakati huo huo Fatma Abdalla Mussa  akisoma risala ya wanawake wa Zanzibar ameitaka serikali kuyafanyia kazi na kuyatafutia ufumbuzi matatizo ya udhalilishaji yanayowakumba   wanawake kama  vile kutelekezwa na watoto,kupigwa,kubakwa, kunyimwa  haki ya kurithi pindi wanapoachika  katika ndoa pamoja na kuondoa wimbi la talaka katika jamii.
Amesema endapo mpango huo utafanya kazi kwa uwadilifu na kufuata  sheria  utaweza  kusaidia  kwa kiasi kikubwa  kuondoa kilio na maumivu ya muda mrefu katika  mioyo ya wananchi.
Nae Katibu mkuu  wizara yakazi,uwezeshaji,wazee,vijana,wanawake na watoto  Fatma Harib Bilali  amesema mpango huo umezingatia sera na sheria za udhalilishaji, kuimarisha mila na desturi za wananchi  kuweka mazingira salama, kuwawezeasha  wanawake kiuchumi,kuweka mifumo mizuri  katika vyombo vya sheria kuhakikisha vitendo hivyo  vinamalizika
Amesema kuzinduliwa  kwa mpango huo utaweza kutela faraja na kuzaa matunda  kwa jamii na serikali na kutoa wito kwa wazazi na walezi  kuwaongoza vyema watoto katika malezi bora.
Kwaupande wa wizara mbalimbali za  serikali ikiwemo wizara ya katiba  na sheria,Wizara ya tawala za mikoa na idara maalum,Wizara ya Afya,Wizara ya elimu,Wizara ya habari  Zanzibar zimeahidi  kutoa ushirikiano  wa hali ya juu katika  kupambana kila mmoja kwa nafasi yake  ili kuuwezesha mpango  huo kufanya kazi  ya kumaliza  ukatili na udhalilishaji  visiwani Zanzibar pamoja na kuzifanyia marekebisho ya baadhi ya sheria zilizokuwa na matatizo ambazo  hukwambia kesi  kushindwa kuendelea  mbele.
Mapema Jeshi la Polisi  limetoa ahadi ya Kuongeza kasi ya upelelezi wa kesi kwakushirikiana na Ofisi ya DPP ili kutoa msukumu  wa kurahisisha  ufatiliaji wa kesi hizo za ukatili na udhalilishaji   na kuisaidia mahakama kuweza kutoa adhabu kali ili  kuwa  fundisho kwa wahalifu.
Askari wa Jeshi la Polisi wasikiliza kwa umakini zaidi  Hotuba ya Rais wa Zanzibabar na mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mh. Ali Muhammed Shein iliosomwa na Waziri wa kazi Uwezeshaji,wazee,vijana,wanawake na watoto Maudline Cyrus Castico.
Uzinduzi huo uliowakutanisha watu zaidi ya mia nne asasi za kiraia,mashirika ya kimataifa,jeshi la polisi watendaji wa mawizara,taasisi za kidini.
chanzo:Zanzibar24

Comments