
Akizungumza kwa niaba ya Katibu Mkuu wa Wizara ya miundombinu na
usafirishaji, katika mkutano wa kuwaelimisha wadau wa sekta ya uchukuzi
juu ya mpango wa Taifa wa utafutaji na Uokozi (SEARCH AND RESCUE PLAN)
mkurugenzi huyo amesema watendaji wa Mamlaka za usafiri watakapofanya
kazi kwa Bidii na sheria watasaidi kupunguza ajali zinazojitokeza.
Amesema kuna Ajali Nyingi zimejitokeza na kusababisha majanga makubwa
kwa wananchi na hasara kwa serikali ikiwemo kuzama kwa meli, hivyo
Serikali ya Zanzibar imekusudia kuweka boti tatu zitakazorahisisha
huduma za Uokozi kwa wakati, katika maeneo ya Bandari ya Mkokotoni
Unguja ,Mkoani pamoja na Wete Pemba.
Kwa upande wao washiriki wa Mafunzo hayo Wameziomba Serikali za
Tanzania kuimarisha mawasiliano ya Vyombo vya Baharini ili watumiaji wa
vyombo hivyo waweze kutoa taarifa kwa wakati wakati wanapokutwa na
majanga wakiwa safarini.
Wamesema majanga mingi yanatokea wakati wanapokuwa safarini na
kushindwa kuripotiwa kwa wakati kutokana na kukusekana kwa mawasiliano
ya uhakika jambo ambalo hupelekea vifo kwa wasafiri na upotevu wa mali.
Nae kaimu mkurugenzi wa Usalama na mazingira katika wizara ya ujenzi
Uchukuzi na Mawasiliano ya Muungano Stela Joshua Katondo ,amesema
kutokana na kuchelewa kwa taarifa za majanga ya Anga na baharini mafunzo
haya yatasaidi upatikana wa taarifa kwa haraka ili waweze kuwaokoa
wasafiri wanapopata matatizo wakiwa safarini.
Amesema mafunzo hayo pia yanaendelewa kutolewa kwa nchi zote za
Africa mashariki ili kuongeza ushirikiano wa uokozi katika nchi hizo,
pamoja na kuwatambua wasafiri watakaopata majanga kupatiwa huduma muhimu
ikiwemo waliofariki kufikishwa kwa familia zao.
Aidha amesema pindipo mpango huo utakamilika utaonesha namna bora na
salama ya uokoaji kwa wasafiri ili waweze kuokoa mali za na maisha wa
watu bila kusababisha upotezo wa rasilimali hizo.
Mafunzo hayo ya siku moja yametowa kwa watendaji wa Mamlaka za Anga
na Usafiri wa Baharini ,watendaji wa Jeshi la Polisi ,Wavuvi ,wizara
zinahusiana na uokozi na uchukuzi pamoja na baadhi ya Viongozi wa wilaya
na mikoa ili waweze kupambana na majanga yanayoweza kujitokeza katika
maeneo yao ya kazi.
chanzo:Zanzibar24.
Comments