
Waziri wa kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto Maudline
Cyrus Castico pamoja na Wawakilishi mbalimbali wa mashirika ya kimataifa
wakisikiliza maswali yanayoulizwa na Waanishi wa Hababari
kuhusu uzinduzi wa vitendo vya ukatili na udhalilishaji wanawake na
watoto Zanzibar.
Akitoa taarifa kwa vyombo vya habari juu ya uzinduzi wa mpango huo
unaotarajiwa kuzinduliwa kesho katika hoteli ya Zanzibar beach resort
Mjini Zanzibar Waziri wa kazi,Uwezeshaji,Wazee,Vijana,Wanawake na Watoto
Maudline Cyrus Castico amesema mpango unalenga kutoa mwongozo kwa
namna ya kumaliza masuala ya ukatili na udhalilishaji kwa wanawake na
watoto visiwani Zanzibar.
Amesema bado wanawake na watoto wanafanyiwa vitendo vya udhalilishaji
siku hadi siku jambo linalopelekea athari kubwa katika kijamii,kiafya
na hata kiuchumi kwa waathirika wa vitendo hivyo.
Castico amesema licha ya juhudi mbalimbali zinazochukuliwa katika
kukabiliana na vitendo hivyo lakini bado kuna changamoto nyingi
zinazorudisha nyuma jitihada ikiwemo uwajibikaji mdogo kwa baadhi ya
watendaji wa masuala ya udhalilishaji,jamii yenyewe kuwaonea muhali
watenda udhalilishaji.
Amesema pia mpango huo utaendeleza kampeni ya kuelimisha umma na
kuhamasisha jamii kushughulikia masuala ya ukatili dhidi ya wanawake na
watoto iliyozinduliwa mwaka 2014 na Rais wa Zanzibar Dr.Ali Mohamed
Shein.
Hata hivyo Castico amesema lengo la Serikali kwa kushirikiana na
asasi za kiraia,mashirika yasiyo ya kiserikali na wadau wa maendeleo ni
kuhakikisha wanavitokomeza vitendo vya aina zote za udhalilishaji pamoja
na kuwachukulia hatua watenda maovu kwa wanawake na watoto hapa
nchini.
Kwaupande wao Wawakilishi wa mashirika ya kimataifa kutoka Save the
Children,UNICEF,UNFPA pamoja na UN WOMEN wamesema kupitia mpango huo
unaotarajiwa kuzinduliwa Zanzibar utasaidia kuondoa kabisa aina zote za
ukatili na udhalilishaji na kuweza kuwapatia heshima wanawake na
watoto.
Wamesema wataongeza ushirikiano kwa serikali na kuunga mkono
mapambano ya ukatili na udhalilisahji ili kumaliza kabisa kadhia hiyo
inayorudisha nyuma maendeleo na kudumaza uchumi wa nchi.
Aidha wamesema mpango huo utaibua mbinu mbadala za kukabiliana na
udhalilishaji endapo jamii ya wazanzibar itatumia busara na kufanya kazi
kwa mashirikiano.
chanzo:Zanzibar24
Comments