SMZ kusitisha rasmin mitambo ya Analogi kuelekea Digital.

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inatarajia kuzima rasmin mitambo yao ya analogi ifikapo tarehe 31 ya mwezi huu na kuwasha digital ili kwenda sambamba na nchi zilizoendelea kimawasiliano.

Zanzibar24 ilifunga safari hadi tume ya utangazaji Zanzibar na kukutana na Mhandisi wa tume hiyo Ali Hussen Ayoub kufahamu undani wa jambo hilo.


Mhandisi aliiyambia zanzibar24 kuwa  Zanzibar itazima mitambo yake ya Analogi ifikapo tarehe 31 na kuwasha Digital licha ya kuwa wamechelewa kwa muda mrefu kulikosababishwa na maboreshe mbalimbali  ya mitambo na mambo mengine.

Amesema ujio wa mitambo mipya ya digital imekuja baada ya makubaliano ya nchi wanachama wa jumuiya ya mawasiliano ya umoja wa mataifa (ITU) kwamba nchi wanachama wote wabadilishe mifumo yao ya kurusha  matangazo ya televisheni  kutoka analogi kwenda digitali ili kuboresha huduma kwa wananchi.

Aidha amesema mifumo ya  digitali itaweza kuleta faraja na maendeleo makubwa kwa wananchi wa Zanzibar kwa  kupata huduma zenye ubora  na uhakika ambapo  kutapungua  gharama za uwendeshaji na kuwataka wananchi kutoa ushirikiano kwa serikali kwani jambo hlilo litaweza kuleta maendeleo.

Hata hivyo amesema bila ya  kupata maendelo ya mifumo ya utangazaji Zanzibar haitaweza  kuendelea hivyo  wananchi lazima wakubaliane na mabadiliko hayo  yenye faida kwani   kutaongezeka  kwa  chanal mbalimbali pamoja na kuongezeka  vituo vya televition  visiwani Zanzibar na kuweza kupata wataalamu wazuri.

Muhandisi wa tume hiyo amewataka wananchi wa Zanzibar  kununua vin’gamuzi ili kupata urahisi na ubora wa hali ya juu na kupata chanali tofauti  na bila ya kununua  kin’gamuzi hawataweza kuonana  kitu katika tv zao.

Amesema  wakiwasha  mitambo ya digitali  tarehe 31  kwa wananchi na mashirika wanaotumia analogi hadi leo hawataona kitu na vifaa vyao vitazima hivyo nivyema wakatafuta njia mbadala mapema ili kwenda sambamba na  nchi zilizoendelea.

Baadhi ya wananchi wa manispaa ya mji wa Zanzibar wametoa maoni yao juu ya ujio wa mitambo mipya ya digital wamesema ni jambo zuri lakini kutokana na hali duni za wananchi watashindwa kumudu gharama za mitambo hiyo.

Wamesema  lazima serikali  iyangalie hali  ya uchumi ya wananchi wake kabla ya kuanza  kwa mitambo hio ya digitali.

“Nijambo zuri  la digitali lakini sisi wananchi hasa wa vijijini inatushinda pesa ya chakula tutaweza kumudu gharama za digital ipo haja serikali ikapunguza gharama za manunuzi ya vin’gamuzi  pamoja na ada ya kila.

chanzo:Zanzibar24

Comments