Serikali ya Korea yaahidi kusaidia ujenzi wa miundo mbinu ya kilimo cha umwagiliaji maji, mkoa wa kaskazini pemba.
Balozi wa jamhuri ya
watu wa korea hapa nchini song geum
young, alisema kuwa, kuimarishwa kwa miundo mbinu hiyo itasaidia kuongeza
uzalishaji wa mpunga kwa wakulima .
Akizungumza na katibu
tawala mkoa wa kaskazini Pemba, huko afisini kwake, Mnazi mmoja Wete, balozi
song geum young alisema, mafanikio
yanaweza kupatikana na kufikia maendeleo yaliokusudiwa, iwapo kutakuwa na
ushirikiano wa wananchi wa Pemba hususani maeneo ambayo miradi hiyo
itatekelezwa.
‘’Ushairikiano ni
muhimu ,wananchi wawe na muamko na kuunga mkono misaada inayowafikia katika
kuendeleza kilimo’’, balozi young alisema.
Sambamba na hayo,
alisema kuwa Serikali hiyo, imelenga kusaidia katika sekta ya elimu kwa
kuchangia madawati, ili kupunguza tatizo la vikalio maskulini.
Naye Katibu Tawala Mkoa wa kaskazini Pemba, Ahmed
Khalid Abdalla, alisema serikali ya mapinduzi ya zanzibar imekuwa ikichukua
hatua za makusudi kuimarisha sekta ya kilimo, ili kuwawezesha wakulima
kuzalisha chakula cha kutosha.
‘’Tunashukuru na
tutashirikiana nanyi kuona kuwa malengo yanafikiwa kwa kuwasaidia wananchi
katika Sekta hii ya kilimo, na kuona kuwa wanajikimu kwa chakula’’, Katibu
Tawala alieleza.
Aidha amesema serikali
ya mkoa itashirikiana na serikali ya jamhuri ya watu wa korea, ili kuona kwamba
utekelezaji wa ujenzi wa mradi huo unakamilika na kuleta tija kwa wananchi .
Hata hivyo katibu tawala
ameitaka serikali ya jamhuri ya watu wa korea kusaidia kuyatangaza maeneo ya
utalii yaliyopo Zanzibar, ili watalii
waweze kutembelea visiwani jambo ambalo litachangia kupatikana kwa pato la
taifa.
Jumla ya dola za
kimarekani milioni kumi zinatatarajiwa kutumika katika kusaidia miundo mbinu ya
kilimo cha umwagiliaji maji kutoka katika ufadhili wa Serikali ya watu wa
Korea.
Comments