Serikali imeanzisha vyuo vya amali ili kusaidia vijana kusoma fani mbalimbali.

Waziri wa elemu na mafunzo ya amali zanzibar mh. Riziki pembe juma amesema serikali imeanzisha vyuo vya amali ili kusaidia vijana kusoma fani mbalimbali ili waweze  kujiajiri.

Mh.  Riziki  ametoa  kauli  hiyo  wakati  akizungumza  na  walimu  na  watendaji  wa  vituo  vya  mafunzo  ya  amali  kwa  kuwataka watekeleze  vyema  dhamana  walizopewa  kila  mmoja  kwa  nafasi  yake  pamoja  na  kuwa  wabunifu  katika  kuitumia  mitaala  wanyofundishia.


Wakielezea  matatizo  yanayowakwaza  katika  kutekeleza  kazi  zao  wafanyakazi  hao  wamesema  ni  pamoja  na  maslahi  duni,uhaba  wa  vifaa  vya  kufundishia  ikiwemo computer,na  ukosefu  wa  huduma  ya  bima  ya  afya  ambayo  ni  muhimu  kutokana  na  vitendea  kazi  hatarishi  wanavyotumia.

Katika  hatua  nyengine  mh.riziki  amekabidhi  hundi  ya  shillingi  million  tano  kwa  kikundi  kinachojishughulisha  na  ufundi  wa  komputer kiliopo  mwanakwerekwe  ambacho  ni  matunda  ya  vituo  hivyo.

Mkurugenzi  mtendaji  mamlaka  ya  mafunzo  ya  amali  bakar  ali  silima  amesema  tayari  wameshatumia  shillingi  millioni  khamsini  kwaajili  ya  kuvipatia    mkopo  vikundi  kumi  vinavyotokana  na  vyuo  hivyo.
 chanzo:Zbc.

Comments