
Kamanda wa Polisi mkoani Mtwara, Neema Mwanga, alithibitisha kutokea
kwa tukio hilo na kueleza kuwa lilitokea juzi saa 2:30 usiku wakati
hakimu huyo akiwa amelala nyumbani kwake maeneo ya Mtandi Kata ya
Mtandi.
Kamanda Mwanga alisema kundi la watu watatu wakiwa na mapanga
walivamia nyumba ya hakimu huyo kisha kuanza kuwasumbua watoto wake
ambao walikuwa nje ya nyumba hiyo, na baada ya Ulaya kusikia sauti za
watoto wake alitoka nje na kukutana na majambazi hao.
Alieleza wakati Ulaya akiwa katika jitihada za kuwaokoa watoto wake
wakiwa mikononi mwa majambazi hao, walianza kumpiga kwa kutumia mapanga
hayo na kumjeruhi katika maeneo mbalimbali ya mwili wake.
Alisema moja ya maeneo ambayo hakimu huyo amejeruhiwa vibaya ni
mikono. na baadae alifanikiwa kukimbia na majambazi hao walifanikiwa
kutoroka.
Kamanda Mwanga alisema watu hao haijajulikana walikuwa na dhamira
gani dhidi ya hakimu huyo na kwamba hawakuchukua mali yoyote ya hakimu
huyo.
Alisema hadi sasa hakuna mtu yeyote ambaye anashikiliwa na polisi
kuhusiana na tukio hilo na kwamba Jeshi la Polisi linaendelea na
uchunguzi na atakayebainika kuhusika atafikishwa katika mkono wa sheria.
Kwa upande wake, Mganga Mfawidhi wa Hispitali hiyo, Dk. George
Kumwembe, alithibitisha kumpokea hakimu huyo akiwa na majeraha na
kupatiwa matibabu ya awali.
Dk. Kumwembe alieleza kuwa hakimu huyo kutokana na hali yake kutokuwa
nzuri, alipatiwa rufani na kupelekwa katika Hospitali ya Peramiho ya
mjini Songea kwa ajili ya kupatiwa matibabu zaidi.
chanzo: zanzibar24.
Comments