
Akitoa
taarifa kwa vyomba mbali mbali vya habari Katibu wa Chama hicho Wilaya ya Chake
chake Nd Saleh Nassor Juma kwa niaba ya kaimu katibu wa Wakilishi na Madiwani
Pemba nd. Mohammed Ali Salim amesema ni ukweli usio fichika kuwa baadhi ya
vyombo vya dola vinatumika vibaya kwa chuki za kisiasa dhidi ya wafuasi wa
chama hicho.
Amesema kuwa
maadhimio hayo siyo tu kuwa yameweka msimamo wa chama kuhusiana na kadhiya
iliyo tayarishwa na serekali zilizopo madarakani yakueleza hujuma dhidi ya vyama vya CUF,
CHADEMA na vile vyote vilivyo undwa na
ukawa.
Katika
taarifa hiyo ya wawakilishi na madiwani wa CUF kwa vyombo vya habari imelaani hujuma
hizo na kuahidi kuendelea kuwaunga mkono na viongozi
wa ngazi zote ndani ya chama
hicho hadi pale ushindi wao utakapo patikana.
Aidha wameahidi
kuwaunga mkono wambuge wanane na
madiwani wawili ambao waliovuliwa uwanachama na mwenyekiti wa chama hicho
anaetambuliwa na msajili wa vyama vya siasa Ibrahim Lipumba pamoja na wenzake kuendelea kuwatambuni kama
wanavyo tambuliwa na baraza kuu la CUF Taifa kuwa bado ni viongozi halili na
wapambanaji ndani ya chama hicho.
Hatahivyo wamewapongeza
wabunge hao pamoja na madiwani kwa ujasiri pamoja na ukakamavu waliounyesha
katika mapambano hayo kwani wanaamini yakwamba ushindi ndani ya chama hicho
utapatikana hivi karibuni.
‘‘sisi hawa
kwetu ni wabunge pamoja na madiwani halili wa chama chetu bali tunahawesabau
kama MAKAMANDA MADHUBUTI na MAKINI
katika mapambano haya na sisi tunaahidi kuwa nao beka kwa beka ''.
Pamoja nahayo
ameeleza kuwa kitendo cha spika wa bunge la Jamhuri ya muungano Mh. Job Ndugai kufanya maamuzi ya kuwafukuza wabunge hao ni
kitendo kisicho zingatia sheria wala ustahamilivu nakuonesha udhaifu mkubwa juu ya
uwongozi wake huku wakiendelea kutupia lawama kwa tume ya uchaguzi ya jamhuri
ya muungano wa Tanzania kuwa nayo imeshiriki katika kukihujumu chama hicho.
Akijibu
maswali ya waandishi wa habari waliotaka kujua juu ya mustakbali na mwelekeo wa
chama hicho Mwenyekiti wa chama cha CUF Wilaya ya micheweni Nd. Rashid Khalid
Salim amesema nguvu za umma ndizo zitakazo amua juu ya mwelekeo wa chama hicho
endapo juhudi za kidiplomasia hazito fanikiwa.
Comments