Ashambuliwa mpaka kufa Chake chake Pemba.

Image result for pemba islandKijana mmoja aliyetambulika kwa jina la Ibrahim Hija Kipenda (28) mkaazi wa msingini chakechake amekutwa amefariki huko ndugu kitu wilaya ya chake chake Mkoa wa Kusini Pemba baada ya kushambuliwa na watu wasiojulikana.

Akithibitisha kutokea kwa tukio hilo Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kusini Pemba  Shekhan Mohd Shekhan amesema baada ya askari akiwemo yeye mwenyewe binafsi kuwasili eneo la tukio walimkuta huyo kijana ameshafariki Dunia.


Akielezea zaidi juu ya tukio hilo amesema kuwa katika uchunguzi wa awali wamebaini kuwa kijana huyo alikua ni mwizi na inaonesha alishambuliwa na watu na yeye Marehemu alikutwa na nazi  na kipolo pamoja na matunda.

Aidha Kamanda Shekhan ameitaka jamii kutojichukulia sheria mikononi mwao na badala yake wafuate sheria ili kuweza kuwafikisha katika vyombo vya sheria na ni kosa la jinai kujichukulia sheria mkononi.

Kwa upande wake Daktari dhamana wa Hospitali ya Chake chake Habibu Khamis amekiri kupokelewa mwili wa Merehemu huyo na uchunguzi umebainisha chanzo cha cha kifo chake ni kutokana na  majeraha makubwa aliyoyapata  ikiwa ni pamoja na kuchomwa kitu chenye ncha kali.

Nae mkuu wa Wilaya ya Chake Chake Mh. Salama Mbarouk Khatib amesema kuwa walipata taarifa ya kuonekana kwa marehemu huyo wakati wakiwa katika maadalizi ya ziara rasmi ya Rais wa Zanzibar hapa Kisiwani Pemba.

Amefahamisha kuwa kwa kushirikiana na vikosi vya ulinzi na usalama vya Mkoa wa Kusini Pemba waliweza kufika katika eneo la tukio na kuuchukua mwili wa marehemu na kuupeleka hospitali ya Wilaya ya ChakeChake kwa uchunguzi baadae mwili huwo kukabidhiwa kwa ndugu wa marehem kwa mazishi.

Comments