ZATU yailalamikia Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

HABARIChama cha Walimu Zanzibar ZATU kimeiomba serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kulipatia ufumbuzi tatizo la mishahara isiozingatia viwango vya elimu  ili Walimu waweze kunufaika na mishahara yao.

Akizungumza na waandishi wa Habari Mjini Zanzibar katibu mkuu wa ZATU Mussa Omar Tafurwa  amesema kwa sasa walimu wamekuwa na mwamko mkubwa wa kujiendeleza kitaaluma ili waweze kutoa elimu bora kwa wanafunzi lakini bado wanakabiliwa na tatizo la mishahara isiozingatia kiwango cha elimu.


Aidha amesema serikali imetekeleza azma yake ya kuengeza mishahara kwa watumishi wa serikali lakini mishahara hiyo imekuwa ikiwanufaisha watu wachache hususani kwa watendaji wa waliochini ya wizara ya elimu.

Hata hivyo amesema mishahara hiyo pia imesababisha baadhi ya wafanyakazi kushushwa ngazi zao za mishahara jambo ambalo linawakosesha kujiinua kimaendeleo na kukosa kuhudumia familia zao.

Hivi karibuni Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imetangaza Viwango maalumu vya mishahara kwa watumishi wa umma ambapo kwa sasa baadhi ya Watumishi wanalamikia kutotolewa kwa kufuata sheria zilizopo.
chanzo:Zanzibar24.

Comments