WWF yaonya mradi wa kawi ya umeme Tanzania.

Mradi  wa kawi ya umeme unaotarajiwa kujengwa katika turathi za Tanzania unahatarisha uhai wa wanyama pori na kipato cha maelfu ya raia wanaotegemea eneo hilo.

Afrika mashariki inatarajia kujenga mradi mkubwa wa kawi katika eneo la Stiegler Gorge ndani ya turathi za UNESCO, katika eneo la uhifadhi wa wanyamapori la Selous kwa dhumuni  la kuimarisha sekta yake ya kawi.


Shirika la kimataifa la uhifadhi wa wanyamapori (WWF) limeonya kuwa njia inayotumiwa na wanyama pori wakati wanapohamia maeneo mengine ita kabiliwa na mradi huo huku watu 200,000 wanaotegemea eneo hilo kwa kipato wakiathiriwa na mradi huo.

Bwawa la umeme linatarajiwa kujengwa katika turathi hizo za UNESCO lenye ukubwa wa taifa la Switzerland ambalo ni maarufu kwa wanyama tofauti.

Rais wa Tanzania John Pombe Magufuli alisema  hakuna pingamizi yoyote itakayo zuia serikali yake kujenga mradi huo.

”Naelewa kwamba mradi huu wa Stiegler Gorge utapingwa na wengi, Utapingwa kwa sababu eti kuna maswala ya mazingira ambayo yanapaswa jkuangaziwa na wengine watasema kwa sababu unajengwa katika mbuga ya uhifadhi wa wanyama pori ya Selous.Mradi huu utakabiliwa na pingamizi chungu nzima lakini nawataka raia wa Tanzania kutahabiti ili kuhakikisha kuwa mradi huu unafanikiwa”.

Mpaka sasa Tanzania ina  idadi ya watu milioni 53 ina Megawati 1400 ya umeme ambapo mradi wa bwawa hilo unakadiriwa kutoa Megawati 2000 za umeme.

Rais  amesema mradi huo utachukua asilimia 3 pekee ya eneo hilo la uhifadhi wa wanyama pori.

Shirika la kimataifa la uhifadhi wa wanyama pori WWF,  linaitaka serikali ya Tanzania  kufanya utafiti wa kina wa mazingira katika eneo hilo ili madhara yote yabainike kabla ya mipango ya mradi huo  unaotarajiwa kugharimu dola bilioni mbili za Marekani kuanza.
chanzo: zanzibar24.

Comments