Akitoa taarifa ya ujenzi wanyumba hizo kwa naibu waziri wa wiazara
ya ujenzi mawasiliano na usafirishaji kaimu mkurugenzi idara ya uratibu
wa shirika la Nyumba Pemba Suleiman Hamad Omar amesema kufuatia
uchakavu uliopelekea kuanza kubomoka nyumba hizo idara yake
itatumia shilingi milioni 62 kwa awamu ya kwanza ambazo zitatumika
kulitengeneza block moja lenye nyumba nane.
Kwa upande wao wananchi wanaoishi katika nyuma hizo wameishukuru
serikali kwa juhudi zake za kuwajali wananchi kwa kuwafanyia
matengenezo nyumba zao kwani zilikuwa katika hali isiyoridhisha .
Nae Naibu Waziri wa Wizara ya ujenzi mawasiliano na usafirishaji Mh:
Mohd Ahmada salim amewataka wakaazi wa nyumba hizo kuzitunza kwa
kuzifanyia usafi ili kuepuka maradhi ya miripuko ambapo kufanya hivyo ni
kumuenzi muasisi wa ujenzi wa nyumba hizo marehemu mzee Abeid Amani
Karume.
chanzo:Zbc.
Comments