Wizara ya Habari Utalii,Utamaduni na Michezo imesema kutokana na
kupotea kwa kiasi kikubwa mila na utamaduni wa mzanzibar visiwani
Zanzibar itahakikisha kupambana na kutoa elimu ili utamaduni wa
mzanzibari usipotee.
Akitoa taarifa kwa Waandishi wa Habari Juu ya siku ya Tamasha la
mzanzibar Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Omar Hassan Omar
Kingi amesema vijana wengi wakizanzibar hivi
sasa wamepoteza utamaduni wao kwa kuiga mila na tamaduni za
kimaharibi jambo ambalo limepelekea kushusha thamani ya
Zanzibar katika utamaduni wake na soko lake la utalii.
Amesema ifikapo tarehe 19 mwezi huu kutafanyika tamasha la
mzanzibari ambalo lengo lake ni kuwashajihisha wananchi na kuona
umuhimu wa kutunza na kulinda mila,desturi na silka zao hasa Zanzibar.
Hata hivyo amesema Serikali imeweka mikakati
imara kuhakikisha inalinda utamaduni wa mzanzibar licha ya
kuwa na muingiliano wa wageni mbalimbali kuja zanziabri
watahakikisha wanakuza Nyanja za utamaduni ili ziende sambamba na
sekta ya utalii ili kukuza mapato ya taifa, kuwapa kipaombele wasanii
pamoja na wazalishaji wa vitu vya utamaduni.
Maadhimisho hayo ya tamasha la Mzanzibar yanatarajiwa kufanyika
ifikapo tarehe 19 mwezi huu katika viwanja vya mnara wa kumbumbu
kisonge na kufunguliwa na Makamo wa Pili wa Rais Balozi Seif Ali Iddi
ambapo ujumbe wa mwaka huu ni Tulinde maadili yetu kupinga
udhalilishaji.
Chanzo:Zanzibar24
Comments