Waziri wa kilimo, mifugo atoa agizo kwa watendaji wa wizara yake kufanya utafiti juu ya maeneo yanayofaa kwa kilimo cha korosho Pemba.
Amesema sehemu hizo zina maeneo mazuri yanayoonesha
kustawi vizuri zao la korosho ambalo na
muhimu duniani.
Agizo hilo
ameliutoa mapema leo huko Giningi Chambani Mkoa wa Kusini Pemba alipokua katika ziara
yake ya siku mbili kisiwani humo na kubahatika kutembelea eneo hilo ambalo
lilikuwa likitumika kwa uchimbaji wa mchanga.
Waziri Hamadi
amesema iwapo wizara itafanya kazi hiyo
kwa ufani mkubwa ya kuipanda mikorosho ya kisasa basi muda
mfupi itaiwezesha serikali kujipotia mapato kupitia zao hilo mbayo yatasaidia
kuendesha shughuli nyengine za kiuchumi.
Sambamba na hayo
waziri huyo ameitaka wizara hiyo kutokuwafumbia macho wale wote ambao
wanahujumu mali asili ambazo ni muhimu katika kujenga uchumi wa nchi yetu hata
kama wapo ndani ya wizara hiyo.
Amesema kuwa
serikali haipo tayari kuona kuwa kuna
badhi ya watu wanazihujumu mali asili na bado wanaendelea kubembelezwa.
Waziri Hamad
ambaye yopo Pemba kwa ziara ya kuangalia utendaji wa wizara yake pia
amebahatika kutembelea katika kiwanda cha kukamua wa mafuta ya halizeti kilichopo Dodeani .
Comments