Waziri Mwakyembe Amtumbua Rasmi Malinzi.....Ni Baada ya Kusitisha Uteuzi wa Mwenyekiti na wajumbe wote wa BMT.
Mwenyekiti
wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) , Dionis Malinzi, ambaye ni ndugu
na Rais wa Shirikisho la Soka Jamali Malinzi ametumbuliwa leo na Waziri
wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mhe. Dkt Mwakyembe
kufuatia agizo la Waziri Mkuu
Waziri
Mkuu Kassim Majaliwa alimtaka Waziri Mwakyembe kupitia baraza hilo na
kulitathimini hivyo baada ya kulipitia na kutathimini amesitisha uteuzi
wa Mwenyekiti wa baraza hilo.
"Kwa
mamlaka niliyopewa na sheria ya BMT Na. 12 ya 1967, nimesitisha uteuzi
wa Mwenyekiti na wajumbe wote wa BMT" amesema Dkt.Harrison Mwakyembe
Kwa
mujibu wa Waziri Mwakyembe amesema kuwa Sekretarieti ya Baraza la
Michezo Tanzania litaendelea na kazi kwa kushirikiana na serikali wakati
mchakato wa kuteua mwenyekiti mpya wa baraza hilo ukiendelea.
chanzo:mpekuziblog.
Comments