
Mratibu wa kitengo cha miguu rungu katika Hospitali Kuu ya Mnazi
Mmoja Dk. Salim Seif Ali alisema kwamba ongezeko hilo linaonesha kuwepo
kwa uelewa miongoni mwa wazazi na walezi wenye watoto wenye matatizo
hayo.
“Mwanzoni tulikuwa tukipokea watoto wawili, watatu, lakini
tuliendelea na kutoa elimu kwa jamii na sasa kumekuwa na mafanikio,
ingawa bado tunaendelea na jitihada za kuwaelimisha wananchi kuhusu
matatizo ya miguu rungu” Alisema Dkt. Salim Seif.
Mratibu wa Klinik hiyo alisema kwamba matibabu wanayotoa kwa watoto
wenye matatizo ya miguu rungu yameonesha mafanikio makubwa kwani kiasi
kikubwa cha walio patiwa matibabu wamepona wameweza kurudi katika hali
za kawaida.
“ZOP wamefanikiwa kwa asilimia 98% japokuwa hakuna
tathmini kamili lakini takribani wote tulio watibu wamefanikiwa
kuondokana tatizo lao la mguu rungu ” aliongeza kusema Dkt, Salim.
Hata hivyo, alisema kuwa mguu rungu si ulemavu bali ni tatizo
linalotokana na mazingira ya mama anayo ishi, lakini chanzo cha tatizo
hilo hakijaweza kufahamika hadi sasa.
Ali sema tatizo hilo linatibika likiwahiwa mapema pale mara tu mama
anapojifungua kuanzia siku moja hadi miaka minne kwa kutumia unga wa
piopio kunyosha mifupa ya mtoto huyo mwenye mguu rungu kwa hatua ya
awali.
Dkt. Salim alisema kitengo hicho kipo mnazi mmoja kwa unguja na
kinatoa matibabu bure bila malipo kwa ushirikiano wa Serikali jumuiya
ya Zanzibar Outreach Program(ZOP).
Akifahamisha kuwa kitengo hicho kinakabiliwa na upungufu wa
wataalamu, na kuishauri Serikali kuweka katika mitaala yake ya elimu
ya afya Mbweni kuingiza somo litalo kabiliana na maradhi hayo ya mguu
rungu pamoja na kufungua matibabu katika hospitali za mikoa kama vile
kivunge na makunduchi kwa unguja ilikuwapunguzia safari ndefu wazazi
kuifuta huduma hiyo mnazi mmoja.
chanzo:zanzibar24.
Comments