Akizungumza na Zanzibar24 Waziri wa Elimu na Mafunzo ya amali Zanzibar Riziki Pembe Juma pamoja na baadhi ya wananchi wamesema bidhaa hizo zilizotengenezwa kwa mwani zinaubora zaidi kwani zinatibu magonjwa mbalimbali.
Amesema Mwani hutengezewa Aina kumi na saba za bidhaa ambapo ni sabuni,mafuta,loshani,saladi,chakula,pia husaidia magonjwa mbalimba ikiwemo maradhi ya ngozi,pia hutia damu hasa mama wajawazito huwasaidia katika kuwajengea afya bora watoto tokea tumboni.
Hata hivyo wamesema kutokana na umuhimu wa zao hilo duniani ipo haja wawekezaji pamoja na wadau mbalimbali kushirikiana na serikali kuwasaidia wakulima wa zao hilo ili waweze kujipatia kipato chao na kuweza kuliinua taifa kiuchumi.
Aidha Riziki amesema Mwani ni zao la tatu kwa Zanzibar kuingiza fedha za kigeni lakini wakulima bado wahajanufaika na kusema kuwa serikali ipo katika mipango ya kuwawezesha wakulima pamoja na kuangalia uwezekano wa kupandisha bei ya zao hilo angalau lifike kilo mia 600 ambalo sasa kilo 300.
chanzo:Zanzibar24
Comments